September 3, 2014

MUSOTI (KUSHOTO) AKIWA MAZOEZINI NA WACHEZAJI WENGINE WA SIMBA.

Hali ya wasiwasi imetanda ndani ya Simba baada ya beki waliyemnasa hivi karibuni, Shafii Hassan, ili kuchukua mikoba ya Mkenya , Donald Musoti, imebainika kuwa usajili wake umegonga mwamba katika Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).
Shafii alisajiliwa hivi karibuni na Simba kwa mkataba wa miezi sita akitokea Ashanti United kwa lengo la kuja kuziba pengo la Musoti alifungashiwa virago ili kumpisha Mganda, Emmanuel Okwi ambaye amejiunga na klabu hiyo wiki iliyopita.
Habari za kuaminika kutoka ndani ya Simba zimedai kuwa jina la mchezaji huyo halikuwemo katika orodha ya majina ya timu hiyo yaliyopitisha na TFF kwa ajili ya msimu ujao wa Ligi Kuu Bara.
Chanzo hicho kilifafanua kuwa inawezekana sababu moja wapo ambayo ilisababisha usajili wa mchezaji huyo kukwama inaweza kuwa ni tatizo la mtandao.
“Usajili wa Shafii umekwama TFF, hivyo hatutakuwa na naye tena katika hatua ya kwanza ya ligi kuu labda mzunguko wa pili.
“Tatizo kubwa la usajili wake kutofanikiwa inawezakana ni kutokana na kuchelewa kupelekwa kwa jina lake TFF ambapo tulilipeleka katika dakika za mwisho kabisa ambazo pengine ‘system’ (TMS), haikuweza kupata data zake kwa wakati husika kutokana na matatizo ya mtandao,” kilisema chanzo hicho cha habari.
Kutokana na hali hivi Simba sasa itakuwa imebakiwa na mabeki wanne wa kati ambao ni Joseph Owino, Joram Mgeveke, Miraji Adam, Isihaka Khatib.
Hata hivyo, Owino ndiye beki pekee kati ya hao mwenye uzoefu wa kucheza mashindano mbalimbali kuliko wachezaji hao ambao ni chipukizi na hawajakomaa kukabiliana na mikikimikiki ya ligi kuu.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic