September 3, 2014


Wakati Yanga ikicheza mchezo wake wa kwanza wa kirafiki jijini Dar es Salaam leo dhidi ya Thika United, Kocha Mkuu wa Yanga, Marcio Maximo, amewakabidhi viungo, Nizar Halfan na Andrey Coutinho jukumu la kupiga faulo.


Maximo amekuwa akiwapa mazoezi ya ziada wachezaji hao ya jinsi ya kupiga faulo wanapokuwa katika programu za mazoezi kujiandaa na ‘mikikimikiki’ ya Ligi Kuu Bara na Kombe la Shirikisho.

Katika mazoezi ya timu hiyo yaliyofanyika jana Jumanne kwenye Viwanja vya Shule ya Sekondari Loyola jijini Dar, Yanga walianza kwa mazoezi mepesi ya kupasha misuli kabla ya Maximo kugawanya wachezaji katika vikosi viwili vilivyoingia uwanjani kucheza soka.

Mara baada ya programu hiyo kumalizika, kocha huyo aliwatenga wachezaji wake ambapo Nizar, Niyonzima na Coutinho walipewa jukumu la kupiga faulo kwa kuwekewa ukuta na ‘rundo’ la wachezaji ila bado kila mmoja alifanikiwa kutikisa nyavu za Dida mara mbili kati ya tatu walizopiga.

Kitendo hicho kinaonyesha wazi kwamba tayari Maximo amewapanga wachezaji maalum kujiandaa na majukumu hayo pindi yatakapotokea katika michezo yao kuanzia huu wa kirafiki unaopigwa leo jijini Dar.

 Licha ya majukumu hayo, Coutinho na Nizar ndiyo wanaoonekana kupewa ‘mzigo mzito’ kwani katika mazoezi ya timu hiyo walipewa jukumu lingine la kupiga kona zote, ambapo zile za upande wa kushoto zilikuwa zikipigwa kwa ustadi na Mbrazil, Andrey Coutinho, huku zinazotokea upande wa kulia zikipigwa na Simon Msuva au Nizar Khalfan.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic