October 28, 2014

SIKU AZAM TV ILIPOSAINI MKATABA WA KUIDHAMINI LIGI KUU BARA

Runinga ya Azam TV yenye asili yake Tanzania, sasa imeingiza maombi ya kutaka kudhamini Ligi Kuu Rwanda.

Azam TV ni kati ya wadhamini wa Ligi Kuu Bara na ndiyo kampuni ya kwanza ya matangazo kuidhamini ligi hiyo nchini.
Habari za uhakika kutoka nchini Rwanda zimeelezwa kuwa Azam TV imekuwa kwenye ushindani mkubwa na Tele 10 inayomiliki TV na redio.
“Kweli kumekuwa na ushindani mkubwa, awali tulielezwa Tele 10 wameshinda lakini tulipofika kwenye mkutano wa waandishi ikashindakana mkataba kusainiwa,” kilieleza chanzo kutoka Rwanda.
“Lakini baadaye tukapata taarifa kwamba mambo yalikwama kwa kuwa Azam TV ya Tanzania imetoa fedha nyingi zaidi.”
Championi Jumatano lilifanya juhudi za kuupata uongozi wa runinga hiyo na Mkurugenzi Mkuu wa Azam TV, Rhys Torrington raia wa Uingereza akathibitisha hilo.
“Sasa ninachoweza kusema ni kwamba tunawania kupata udhamini wa Ligi Kuu Rwanda.
“Tunafanya hivyo kama kampuni nyingine za Rwanda zinavyotaka nafasi hiyo,” alisema huku akisisitiza hana ufafanuzi zaidi kwa kuwa wanasubiri majibu.

Kama itafanikiwa kupata udhamini huo, Azam TV itaweka rekodi kuwa kampuni ya kwanza ya Tanzania kudhamini ligi ya nje.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic