October 4, 2014


London, ENGLAND
UTAMU wa Ligi Kuu England haushuki, maana kila wiki kuna kazi ya aina yake ambayo inakuwa na burudani ndani yake.
Mechi za wiki iliyopita zilikuwa zenye mvuto wa juu ukizingatia kulikuwa na mbili za watani wa jadi.
Leo na kesho, halikadhalika ni mechi ambazo si lahisi kujua ni nani ataibuka mshindi, mfano zile za Sunderland dhidi ya Stoke City au Liverpool inayochechemea dhidi ya wabishi Wes Brom, zote zitapigwa leo.
Kesho ndiyo kibarua hasa,zitakazopigwa ni nne, lakini mbili Chelsea dhidi ya Arsenal na
Achana na Man United wanaopambana na Everton, kila mmoja atatamani kukaa kwenye runinga na kuangalia.
Wakati timu zote zinashuka uwanjani, rekodi zinaonyesha kuna timu zenye rekodi nzuri nyumbani, nyingi zina uwezo wa juu hata ugenini.
Timu hizo ndiyo zinafanya ligi iwe na mvuto zaidi kwa kuwa zinaongeza ugumu na kuifanya isitabirike, kwamba wakati wowote zinashinda tu bila ya kujali ziko ugenini.
Hizi hapa ni timu tano zilizofanikiwa kuingia kwenye tano bora ya zilizoshinda nyumbani na ugenini, au upande mmoja kati ya hiyo kutokana na ushindi au sare ilizozipata katika mechi sita za Ligi Kuu England.
Chelsea:
Chelsea ndiyo inaonekana iko vizuri zaidi, nyumbani au ugenini, inashinda tu. Imeshinda mechi zake zote tatu za nyumbani na kubeba pointi tisa, halafu ikashinda mbili na sare moja ugenini, haijapoteza kokote.
Southampton:
Southampton imeshinda mechi mbili za nyumbani, sare moja, haijapoteza. Ugenini ikashinda mbili pia na kupoteza moja tu. Hii inaonyesha ina kikosi imara pia, ila ‘pumzi’ yake kadiri ligi inavyosonga ndiyo itatoa majibu.

Man City:
City iko safi pia, maana ugenini imeshinda mechi mbili katika tatu ilizocheza. Lakini mambo si mazuri sana nyumbani kwa kuwa imechza naonyesha kuwa na kikosi imara pia, katika mechi tatu za nyumbani, ina sare moja, imeshinda moja na kupoteza moja.


Aston Villa:
Wakali ugenini, maama katika tatu, wameshinda mechi mbili. Ila nyumbani ndiyo mambo hayajaa ‘fresh’ maana wameshinda moja, sare moja na kupoteza moja. Hata hivyo si wastani mbaya sana kwa kuanza.
Arsenal:
Nao wako vizuri lakini si sana, katika mechi tatu za ugenini wameshinda moja na sare mbili, maana yake hawajapoteza nje ya Emirates. Lakini waliporudi katika dimba la kwao, wakashinda moja na kutoka sare mbili pia.

MSIMAMO WA NYUMBANI:
                                           P         W         D       L        GF      GA     Pts
1         Chelsea                 3         3         0         0         9         2         9
2         Southampton      3         2         1         0         6         1         7
3         Man United          3         2         0         1         7         3          6
4         Swansea City       3         2         0         1         4         1         6
5         Leicester City      3         1         2         0         8         6         5

MSIMAMO WA UGENINI:
                                            P         W        D        L         GF     GA       Pts
1         Chelsea                  3         2         1         0         10         5         7
2         Man City               3         2         1         0         8         4         7
3         Southampton       3         2         0         1         5         3         6
4         Aston Villa            3         2         0         1         2         3         6
5         Arsenal                   3         1         2         0         6         3         5


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic