October 4, 2014


Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Mwesigwa Celestine , amesema kuwa malalamiko juu ya changamoto za mfumo mpya wa matumizi ya tiketi za kielektroniki yamefika mezani kwake na akasisitiza kuwa tayari wameanza kulifanyia kazi suala hilo.


Kumekuwa na malalamiko ya mfumo huo wa tiketi ikiwemo kulanguliwa, pia kuwepo na mashine chache za kutolea huduma hiyo uwanjani jambo linalofanya baadhi ya mashabiki kutoingia uwanjani kwa muda muafaka kuzisapoti timu zao.

Mwesigwa amesema malalamiko juu ya mfumo huo wameyapata na wameyafikisha sehemu husika ambapo ni CRDB ili kuweza kuyatafutia ufumbuzi na kusisitiza kuwa tatizo hilo litamalizika katika michezo michache ya hivi karibuni.

“Hili tatizo nikiri tu lipo maana malalamiko yapo mengi na yametufikia walengwa, tulichokifanya ni kuwasiliana na watoa huduma (CRDB) na kuwafikishia ambapo wametuhakikishia watalipatia ufumbuzi ndani ya muda mchache tu, hivyo tunaomba tu mashabiki wawe na subira maana teknolojia hii ni mpya hapa kwetu.


“Jambo jema ni kwamba CRDB wameonyesha ushirikiano mkubwa katika hilo na kuahidi ‘kuimprove’ huduma yao ili wadau wa soka waendelee kuona burudani na kuzisapoti timu zao bila tatizo,” alifafanua Mwesigwa.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic