October 29, 2014

Kipa wa Costal Union ya Tanga, Shabani Kado, amehuzunishwa na kifo cha aliyekuwa kipa wa timu inayoshiriki Ligi Kuu ya Afrika Kusini, Orlando Pirates na timu ya taifa ya nchi hiyo, Senzo Meyiwa.


Senzo alifariki alfajiri ya juzi Jumatatu kwa kupigwa risasi na watu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi.


Kado amesema kuwa ameshtushwa na kifo hicho cha ghafla cha mlinda mlango huyo ambapo kwa upande wake alikuwa anamuangalia kama kipa ambaye atakuwa tishio hapo baadaye na alikuwa anajifunza kupitia kwake.



Aliongeza kuwa, yeye kama mlinda mlango ataendelea kumkumbuka kipa huyo na kwa kumuenzi, atahakikisha anafuata nyendo zake kwa kukaa imara langoni.

“Kifo chake nimekipokea kwa masikitiko makubwa kwani alikuwa ni mmoja wa walinda mlango waliokuwa wanakuja kwa kasi na ataendelea kukumbukwa na wapenzi wengi wa soka hapa Afrika.

 “Nitamuenzi kwa kuhakikisha nafuata nyendo zake ambapo alipokuwa akikaa lango basi ilikulazimu ufanye kazi ya ziada kuweza kumfunga,” alisema Kado.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic