October 4, 2014


Bosi wa benchi la ufundi la Yanga,Marcio Maximo, amesema kuwa haiandai timu kwa ajili ya kuifunga Simba tu bali ni kwa timu zote shiriki za Ligi Kuu Bara ili afanikishe malengo yake ya kutwaa ubingwa huo.


Yanga inakutana na Simba Oktoba 18, kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam ukiwa ndiyo mchezo wao wa nne wa ligi.

Mechi hiyo inatarajiwa kuwa na upinzani mkubwa kutokana na kila timu kutaka heshima huku kila moja ikijivunia usajili wake ilioufanya msimu huu.

Lakini Maximo amesema  wala haufikirii mchezo huo kabisa, zaidi anafanya maandalizi ya kukiboresha kikosi chake kilichofungwa mchezo mmoja dhidi ya Mtibwa Sugar huku wakishinda mmoja na Prisons.

Maximo alisema, sera yake ni kuhakikisha wanashinda kila mechi watakayocheza msimu huu ili kujiwekea mazingira mazuri ya kutwaa ubingwa wa ligi kuu unaoshikiliwa na Azam FC inayofundishwa na Mcrameroon, Joseph Omog.
 “Naandaa timu siyo kwa ajili ya Simba, isipokuwa kwa kila timu nitakayokutana nayo.

“Simba ni moja ya timu nitakazocheza nazo, hivyo ninaendelea kukiandaa kikosi changu kwenye mazoezi yangu ya kila siku, hiyo mechi ya Simba siifikirii kabisa,” alisema Maximo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic