October 4, 2014


Mshambuliaji mpya wa Simba, Elias Maguli, amepewa majukumu ya kiungo mshambuliaji Mkenya, Paul Kiongera katika kipindi chote atakachokaa nje ya uwanja.


Hiyo ni baada ya Kiongera kupata majeraha ya goti wakati timu yake ilipocheza mchezo wa kwanza wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Coastal Union baada ya kugongana na kipa wa timu hiyo, Shaaban Kado kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Mkenya huyo, awali kabla ya kuanza ligi kuu alichaguliwa kuwa ‘super sub’ na kocha mkuu wa timu hiyo, Mzambia, Patrick Phiri, anayekinoa kikosi hicho, anatarajiwa kukaa nje ya uwanja miezi miwili akiuguza majeraha ya goti.
Phiri amesema kuwa majukumu aliyokuwa anayafanya Kiongera sasa amemkabidhi Maguli.

Phiri alisema, majukumu ya Maguli anayotakiwa kuyafanya ni kuusoma mchezo wakati yupo benchi kabla ya kuingia kuubadili akitokea nje ya uwanja kama ‘super sub’.

Aliongeza kuwa, anaendelea kumuandaa mshambuliaji huyo kwenye mazoezi yake ili kuhakikisha anashika maelekezo anayompa na kuyafanyia kazi kwenye mechi.

“Kabla ya Kiongera kupata majeraha ya goti, nilikuwa namtumia kama ‘super sub’ kwa ajili ya kubadilisha mchezo akiwa nje kwenye benchi langu.

“Nilifanikiwa kwa Kiongera kumbadilisha kutoka kwenye kikosi changu cha kwanza na kumuandaa kuwa ‘super sub’ na ndivyo nitakavyofanya kwa Maguli,” alisema Phiri.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic