October 28, 2014



 Kocha Patrick Phiri wa Simba amesema matokeo ya sare mfululizo yanamuumiza sana.

Lakini akasisitia ndiyo wakati mwafaka ambao Wanasimba wanapaswa kutulia na kutafuta jibu sahihi la tatizo.
“Hakuna anayefurahia haya matokeo, najua mashabiki na viongozi wanaumia sana. Lakini makocha na wachezaji pia tunaumia.
“Hali si ya kawaida, lakini tunapaswa kutulia badala ya kulumbana, tuangalie tatizo na mwisho tutafanya vizuri,” alisema Phiri.
Simba imetoka sare tano mfululizo, hali ambayo imezua zogo kubwa miongoni mwa Wanasimba.

Katika mechi zote tano ilizotoka sare, Simba imetangulia kushinda halafu wapinzani wao wakasawazisha.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic