October 28, 2014



Kocha wa zamani wa Simba, Talib Hilal ambaye anafanya kazi zake nchini Oman amesema kuwa ni mapema sana kwa Simba kuanza kulumbana sasa.

Hilal ambye pia aliichezea Simba akiwa mmoja wa mabeki visiki, amesema Simba wanapaswa kukumbuka ligi ndiyo imeanza.
Katika mahojiano maalum na SALEHJEMBE, Hilal amesema Simba ina kikosi chenye wachezaji wengi wapya.
“Wanahitaji muda, haraka haitawezekana hata wafanyeje. Vizuri watumie muda mwingi kuwajenga kisaikolojia, natumai hawatakuwa na tatizo la kiufundi kubwa.
“Lakini vizuri pia kumpa kocha nafasi, lazima wakumbuke ana muda gani tokea amechukua timu hiyo mpya.
“Kingine waangalie wana majeruhi kadhaa wamejitokeza, hivyo wajue lazima kuna upungufu unatokea na lazima ushughulikiwe kwa kufuata utaratibu mzuri,” alisema ambaye ni Kocha wa timu ya taifa ya ufukweni ya Oman.

Hilal ndiye aliipa Simba ubingwa wa Ligi Kuu Bara (ligi ndogo) mwaka 2008, kikosi chake kikiishinda Yanga ya Sredojevic Milutin ‘Micho’.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic