October 5, 2014


Wakati fulani, aliyekuwa kocha wa Real Madrid, Jose Mourinho aliwahi kutoa kauli hii: “Kama hauna mbwa, basi unalazimika kuwinda hata na paka.”

Ilionekana ni kama dharau kwa mshambuliaji Karim Benzema, akinaanisha hana sifa za kuwa namba tisa sahihi.
Kauli hiyo ya Mourinho imekuwa ikizua mijadala ya kila aina kuhusiana na ubora wa Benzema.
Lakini takwimu sasa zinamlinda na kuonyesha Benzema ni bora hata kuliko Gonzalo Higuaín. Benzema alifunga mabao 26 baada ya kucheza mechi 57 za msimu uliopita lakini akafanya vizuri zaidi katika mechi zenye presha kubwa dhidi ya Barcelona.

Kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya ndiyo usiseme, takwimu zinaonyesha Benzema amefunga mabao 38 katika mechi 67 alizocheza.
Mabao yanamfanya awe na wastani wa 0.57 ya bao kwa kila mechi.
Ajabu wako hadi sasa wanahoji uwezo wake, wakati wanamuita mshambuliaji mpya wa Atletico Madrid ambaye alikuwa Bayern Munich  Mario Mandzukic, kuwa ni aina ya mfungaji bora kwa upande wa washambuliaji.
Mandzukic yeye amefunga mabao 18 katika mechi 53 za Ligi ya Mabingwa Ulaya na kumpa wastani wa 0.34 ya bao kwa mechi ambayo ni chini ukilinganisha na ile ya Benzema.

Hii inaonyesha kiasi gani wako wale ambao wamekuwa hawampendi tu Benzema au ana bahati mbaya kwani kwa takwimu, zinaonyesha ni mmoja wa washambuliaji bora kabisa duniani.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic