November 24, 2014


Wakati harakati za usajili kwa timu za Ligi Kuu Bara zikizidi kushika kasi, mambo yanaonekana kumwendea vibaya kipa wa Simba, Hussein Shariff ‘Casillas’ ambaye muda wowote anaweza kufungashiwa virago vyake klabuni hapo.

Kipa huyo ambaye alijiunga na Simba hivi karibuni akitokea Mtibwa, tangu atue klabuni hapo, ameshindwa kuonyesha ubora wake wa msimu uliopita uliomfanya atwae tuzo ya kipa bora wa ligi kuu msimu huo.

Taarifa kutoka ndani ya Simba zimeeleza uongozi unaangalia uwezekano wa kuachana na kipa huyo kutokana na kushindwa kuonyesha makali yake katika mechi chache alizoitumikia, kabla ya kuumia mguu.

Pia hofu ya kuwa majeruhi inawapa hofu, ingawa anaweza akabaki kama Simba haitaongeza kipa mwingine.

“Ukiachana na kiwango lakini pia kuna mambo ambayo amekuwa akiyafanya ambayo yamekuwa hayawapendezi viongozi pamoja na baadhi ya wachezaji wenzake.

“Hivi sasa Casillas hazungumzi na Ivo Mapunda, sababu kubwa iliyosababisha wafikie hali hiyo ni mambo ya ushirikina, kila mmoja anamtuhumu mwenzake, jambo ambalo linaweza kusababisha balaa katika kikosi chetu.

“Kutokana na hali hiyo uongozi umeona ni bora uachane na Casillas ili kuepusha matatizo zaidi ambayo yanaweza kujitokeza hapo baadaye endapo ataendelea kubakia klabuni hapo,” kilisema chanzo hicho cha habari.


Ofisa Habari wa Simba, Humphrey Nyansio alipoulizwa juu ya mpango huo wa kutaka kumfungashia virago Casillas, hakuwa tayari kuzungumza lolote juu ya suala hilo zaidi ya kusema: “Sijapata taarifa yoyote kuhusiana na suala hilo.”

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic