November 10, 2014


Mshambuliaji Mnigeria, Emeh Godwill Izuchukwu, amesema anataka kurejea Simba na kuendelea kuichezea huku akiahidi mabeki Ligi Kuu Bara watayaona maajabu yake.


Mshambuliaji huyo wa zamani, sasa anakipiga katika timu ya daraja la pili ya Elverum FC ya nchini Norway.

Izuchukwu, raia wa Nigeria, tayari amepiga simu nchini na kuwasiliana na mmoja wa rafiki zake ambaye ni mwanasheria ambaye inaelezwa amewasiliana na viongozi wa Simba akitaka kurejea nchini.

Hata hivyo, uongozi wa Simba bado haujatoa msimamo ingawa inaelezwa huenda akarejeshwa kuongeza nguvu kwenye safu ya ushambuliaji.

Izuchukwu anaweza kurejeshwa kwenye dirisha dogo la usajili linalofunguliwa Jumamosi ijayo.

Mnigeria huyo akiwa na Mnigeria mwenzake, Orji Obina waliichezea Simba miaka minne iliyopita na kuwa miongoni mwa washambuliaji hatari.

Hata hivyo, aliondoka nchini kwenda Sweden ambako alijiunga na Klabu ya Enkoping na baadaye Assyriska FC kabla ya kuondoka Sweden na kutua Ranheim IL ya Norway.

Phiri, Poulsen wapanga mabegi Dar, Denmark
Poulsen apanga mabegi Denmark, Phiri apanga Dar

Na Ezekiel Kitula

MAKOCHA Patrick Phiri na Kim Poulsen, kila mmoja ameanza kupanga mabeki kwa wakati wake kwa malengo tofauti.

Phiri anajiandaa kuondoka Simba kwenda likizo kwao Zambia baada ya Ligi Kuu Bara kusimama huku akiwa ameiongoza Simba kushinda mechi moja kati ya saba.

Lakini Poulsen ambaye amefanya mazungumzo na Simba, anapanga mabegi yake kujiandaa kutua nchini wakati wowote kuchukua nafasi ya Phiri ambaye inaelezwa hatarejea tena nchini.

Ligi itaendelea tena Desemba 26, baada ya kusimama rasmi jana.

Habari kutoka ndani ya Simba zimeeleza kuwa kuna mkanganyiko katika jambo hilo kuhusiana na Phiri na Poulsen.

“Kidogo linachanganya, lakini Phiri akiondoka, sidhani kama atarejea, ni suala la kujua baadaye. Lakini Poulsen pia yuko tayari kuja,” chanzo kilieleza.

Simba imeamua kuongeza nguvu na kufanya marekebisho kwenye benchi la ufundi kwa kumleta Poulsen aliyewahi kuinoa Taifa Stars.

Lakini kuna baadhi ya wajumbe wa kamati ya utendaji wameonyesha kutofurahishwa na jambo hilo huku wakisisitiza Phiri aendelee kubaki.



Kisiga in, Kiemba, Chanongo out

Kiemba, Chanongo bye bye Simba
#Kisiga arudishwa 
Sweetbert Lukonge na Wilbert Molandi
BAADA ya mchakato wa kuchanganua mambo, kuna asilimia kubwa Kamati ya Utendaji ya Simba ikatoa majibu ya kuwaondoa wachezaji wawili, Amri Kiemba na Haruna Chanongo.

Lakini kiungo mkongwe, Shabani Kisiga anapewa nafasi ya kuendelea kuitumikia timu hiyo kutokana na utetezi wake.

Watatu hao walisimamishwa kwa tuhuma za utovu wa nidhamu na kucheza chini ya kiwango na baadaye wakaonyesha utovu wa nidhamu kwa kushindwa kutokea kwenye kikao cha viongozi.

“Wachezaji walivyojieleza, inaonekana Kisiga amekuwa hana matatizo makubwa na hata imefikia kwamba atasamehewa.

“Lakini Kiemba na Chanongo, kuna zaidi ya asilimia tisini wataondoka Simba. Sijui, labda mambo yabadilike tena mwishoni, si unajua uongozi ni kitu cha watu wengi,” kilieleza chanzo.

“Watu wengi hawajui uongozi unafanya nini, ukweli ni kwamba uongozi unajua kila kitu, unajua mambo mengi kuliko watu wanavyojua na wala hauna nia ya kumuonea mtu, lengo kuisaidia timu.”

Uongozi wa Simba, bado haujatangaza lolote kuhusiana na hilo lakini utakuwa na nafasi ya kumalizia uamuzi huo na kuutangaza ndani ya wiki hii.

Mara baada ya mchezo wa jana ambao Simba walipata ushindi wa bao 1-0 dhidi Ruvu Shooting, Kisiga pekee ndiye alishuka chini baada ya mchezo kumalizika na kwenda kuwapongeza wachezaji wenzake vyumbani.

Hata hivyo, kocha wa Simba, Patrick Phiri, alipoulizwa kama suala lake limekwisha, alisema waulizwe viongozi.

Fin.

Mwadui, Villa zatesa daraja la kwanza
Nasor Gallu na Alpha Amos
TIMU ya Villa Squad ya Dar es Salaam na Mwadui ya Shinyanga, jana zilifanikiwa kushinda mechi zao za Ligi Dara la Kwanza.

Villa inayonolewa na kocha Habib Kondo, ilifanikiwa kushinda mabao 2-1 dhidi ya African Lyon katika mtanange uliopigwa Uwanja wa Karume. Mabao ya Villa yalifungwa na mshambuliaji wa zamani wa Simba na Yanga, Pius Kisambale dakika ya 19 na 87 huku la Lyon likiwekwa kimiani na Omari Ramadhani dakika ya 72.

Nayo Mwadui inayonolewa na kocha Jamhuri Kihwelo ‘Julio’, iliendeleza wimbi la ushindi baada ya kuichapa Green Warriors kwa mabao 2-0 kwenye Dimba la Mwadui, Shinyanga.

Mabao ya Mwadui yalifungwa na  Bakari Kigodeko dakika ya nane na Said Sued dakika ya 17.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic