November 10, 2014


Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete, amesema baba yake mzazi ndiye alisababisha awe shabiki wa Yanga.


Kikwete ameyasema hayo katika mahojiano yaliyorushwa na E FM jana na kusema alipomuona baba yake akiishangilia Yanga, naye akamfuata.

“Baba yangu alikuwa ni Yanga, basi na mimi nikaamua kuwa Yanga na kuanzia siku hiyo nimekuwa nikiiunga mkono.

“Kwa nje ya Tanzania mimi ni shabiki wa Newcastle ya England. Aliyenivutia kuanza kuishabikia ni Alan Shearer.

 “Wakati naanza kuishangilia Newcastle kilikuwa ni kipindi ambacho Shearer anatamba sana,” alisema Kikwete na kuongeza:

“Kwa watoto wangu wako huru kushangilia timu wanazozitaka. Mfano kwa nje ya Tanzania, wako wanaoshangilia Liverpool, Manchester United na Chelsea, hivyo niko pekee ninayeishangilia Newcastle.”

Kikwete ndiye rais mwanamichezo zaidi wa Tanzania katika awamu zote nne za uongozi nchini.

Ndiye rais pekee ambaye alichukua uamuzi wa kutoa fedha kumlipa kocha wa timu ya soka ya taifa, Taifa Stars.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic