November 10, 2014


Kocha Msaidizi wa Kagera Sugar, Mlage Kabange, amelazimika kuiacha timu hiyo kwa muda kufuatia kurudi darasani kwa ajili ya kujiendeleza kielimu.

Kagera Sugar ambayo inanolewa na kocha mkuu, Jackson Mayanja wa Kenya, imedumu na Kabange kwa muda mrefu na makocha wengi wamekuwa wakija na kuondoka huku wakimuacha Kabange.
Kabange amesema amelazimika kuachana na timu hiyo kwa muda kwa ajili ya kurudi darasani katika kujiendeleza na masuala ya ukocha mkoani Morogoro.
“Nipo mkoani Morogoro kwenye kozi fupi ya ukocha ya wiki mbili na timu nimeiacha na kocha Mayanja, hivyo nitarudi baada ya kumaliza kozi yangu.

“Lengo langu ni kuendeleza elimu yangu ili nikirudi niweze kuwa bora zaidi, kuhusu ligi ni ngumu kwa kuwa kila timu imejipanga ipasavyo kuhakikisha inashinda na kusonga mbele,” alisema Kabange.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic