November 10, 2014


Kiungo mchezeshaji wa Yanga, Mnyarwanda, Haruna Niyonzima, amesema hafurahii maisha anayoendelea nayo kwenye timu hiyo na kufunguka kuwa hataongeza tena mkataba wa kuendelea kubaki Jangwani.
Mnyarwanda huyo anayeichezea timu ya taifa ya Rwanda, alijiunga na klabu hiyo msimu wa 2012/2013 akitokea APR ya nchini kwao.


Kiungo huyo, hivi sasa anaruhusiwa kufanya mazungumzo na klabu nyingine anayotaka kwenda kuichezea kutokana na mkataba wake kubakiza miezi sita.

Niyonzima amesema hajui sababu ya kocha wake Mbrazili, Marcio Maximo kumtoa kwenye mechi nne mfululizo za ligi kuu dhidi ya Simba, Stand United, Kagera Sugar na Mgambo JKT, zote katika kipindi cha pili, bila kuambiwa sababu.
Niyonzima alisema, yeye ni mchezaji mkubwa, ni vyema akaambiwa sababu ya kutolewa na kocha wake ili ajue tatizo ni lipi kwa ajili ya kujirekebisha.
Aidha alisema, pia amechoshwa na uzushi unaosambazwa na baadhi ya viongozi na makomandoo wa timu hiyo za yeye kushawishiwa kusaini Simba na kipa namba mbili wa timu hiyo, Juma Kaseja.
Aliongeza kuwa, hali hiyo inamfanya akose amani ya kubaki kuendelea kuichezea Yanga, hivyo amepanga kurejea kucheza ligi kuu ya nchini kwao mara baada ya mkataba wake kumalizika.
“Kiukweli kabisa nimechoka kuichezea Yanga kutokana na sababu mbalimbali. Kwa mfano kocha amenitoa kwenye mechi nne mfululizo za ligi kuu dhidi ya Simba, Stand United, Kagera Sugar na Mgambo bila kuniambia sababu ili nijue tatizo langu nijirekebishe, hali hiyo inanifanya nichanganyikiwe kabisa.
“Mimi ujue ni mchezaji mkubwa ninayeitumikia timu yangu ya taifa, pia ni tegemeo katika timu yangu, ninayecheza dakika zote 90, sasa iweje Yanga niwe natolewa katika kipindi cha pili?

“Kingine kikubwa kinachonichosha kubaki Yanga ni uzushi ninaosambaziwa kutoka kwa baadhi ya makomandoo kuwa Kaseja ananishawishi niende kusaini Simba, kwa kuwa ninalala chumba kimoja naye kila tunapokuwa kambini,” alisema Niyonzima.

1 COMMENTS:

  1. Ndio tatizo la wachezaji wenye ubinafi kama wewe,Ucheze wewe tu na wenzio wasipate nafasi ya kucheza?Sababu zako hazina msingi na unaonyesha umechoka kuitumikia yanga,ruksa kwenda unakojisikia kwenda,Ila asante sana.

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic