December 12, 2014


Mwandishi Wetu, Zanzibar
Habari nzuri kwa mashabiki wa Simba, kiungo mkabaji wa timu hiyo, Jonas Mkude, ameanza mazoezi baada ya kupona malaria iliyomuweka nje ya uwanja kwa wiki moja kwa ajili ya matibabu.


Kiungo huyo alishindwa kumalizia mazoezi ya wiki iliyopita kwenye Uwanja wa TCC, Chang’ombe jijini Dar es Salaam baada ya kutapika kabla ya kufanyiwa vipimo na kukutwa na malaria na kuanza dozi.

Katika mazoezi ya jana yaliyofanyika kwenye Uwanja wa Chuo cha Ualimu hapa Unguja, Zanzibar kiungo huyo alionekana akianza mazoezi mepesi ya binafsi kukimbia akiwa chini ya uangalizi wa daktari, Yassin Gembe.

Gembe alisema Mkude amepona kabisa na mechi ya kesho Jumamosi ya Nani Mtani Jembe dhidi ya Yanga atakuwepo uwanjani kama kocha ataamua kumtumia.

“Mkude kama unavyomuona hii leo (jana) asubuhi ameanza mazoezi mepesi ya binafsi kwa ajili ya kurudisha afya yake ya kawaida, ameanza mazoezi mepesi na baadaye akafanya ya nguvu pamoja na wenzake.

“Ametokea kwenye malaria, hivyo ni lazima aanzie na mazoezi mepesi ili hali ya kawaida irejee, kocha akiamua kumtumia ni ruksa. Tofauti na Mkude hakuna majeruhi mwingine,” alisema Gembe.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic