December 3, 2014


Shabiki mmoja wa Klabu ya Yanga ambaye jina lake halikupatikana haraka, ‘alikunwa’ na uwezo wa mlinda mlango wa timu hiyo, Deogratius Munishi ‘Dida’ na kujikuta akipagawa na kuamua kumkodishia bodaboda staa huyo.


Hayo yalijiri mara baada ya programu ya mazoezi ya Yanga yaliyofanyika wikiendi iliyopita kwenye Viwanja vya Shule ya Sekondari Loyola, Dar ambapo wachezaji wa timu hiyo walikuwa ‘wakichomoka’ kwenda kwao.

Programu hiyo ilipomalizika, wachezaji walikuwa wakitoka uwanjani hapo kila mmoja akiwa na usafiri wake, lakini Dida alipotoka kwenda kutafuta usafiri, shabiki huyo alijitokeza na kumlipia bodaboda.

“Wewe bodaboda chukua pesa hii, mpeleke huyu jamaa tena kwa mwendo wa kifalme, tuna mechi na Simba inakaribia.

“Umfikishe hadi Jangwani, sasa ole wako ukamshushie Msimbazi,” alibwata shabiki huyo huku akimkabidhi dereva wa bodaboda noti ya shilingi elfu mbili.


Mara baada ya makabidhiano hayo, Dida alidandia bodaboda na safari ikaanza kwa mwendo wa taratibu.

SOURCE: CHAMPIONI

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic