Yanga inashuka uwanjani ndani ya muda mchache
ujao kuwavaa Azam FC katika mechi ya Ligi Kuu Bara.
Mechi hiyo kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es
Salaam inasubiriwa kwa hamu kubwa na Yanga wakiwa na rekodi ya kuifunga Azam FC
mabao 3-0 katika mechi ya Ngao ya Jamii. Je, leo wataendeleza ubabe au Azam FC
watalipa kisasi?
Kunaweza kukawa na maswali mengi sana, lakini
burudani kubwa ni ile kati ya mafowadi wakali wa Yanga dhidi ya mabeki wa Azam
FC.
Hakuna ubishi Azam FC ni moja ya timu zenye
mabeki bora katika Ligi Kuu Bara na sasa wameongezewa nguvu mpya.
Kwanza walikuwa na watu hawa watatu imara kama
chuma. Nahodha Aggrey Morris, David Mwantika na Said Morad. Kati ya hao wawili
wakicheza, basi ujue kazi ipo.
Lakini sasa Serge Wawa kutoka Ivory Coast
ambaye ni mzoefu, ameongeza nguvu zaidi na kuifanya Azam FC kuwa na ukuta chuma
kabisa.
Yanga wanaweza kujivunia washambuliaji wao
wawili wapya kabla ya kujumlisha wale wa awali.
Amissi Tambwe, huyu alikuwa mfungaji bora wa
Ligi Kuu Bara kabla ya Simba kumtema msimu huu. Lakini Yanga ina Kpah Sherman
raia wa Liberia.
Huyu jamaa yuko sawa kweli kwa mujibu wa
takwimu za mechi ya Bonanza la Nani Mtani Jembe dhidi ya Simba.
Ingawa hakumaliza, lakini alionyesha ni ‘shoka’.
Swali, leo ataweza kuendeleza alichokifanya siku ile?
Je, Azam FC wataweza kuwazuia wawili hao
ukijumlisha na Mrisho Ngassa, Simon Msuva na wageni wengine wawili, Haruna
Niyonzima raia wa Rwanda na Andrey
Coutinho wa Brazil?
Lazima burudani itakuwa tamu na si hapo, hata
washambuliaji wawili wa Azam FC, Didier Kavumbagu raia wa Burundi ataungana na
Kipre Tchetche wa Ivory Coast.
Kazi itakuwa kwa safu ya ulinzi ya Yanga
itakayoongozwa na Kelvin Yondani ‘Cotton’.
Lazima itakuwa ni mechi yenye burudani kuanzia
kwenye ulinzi, kiungo na ushambulizi. Vizuri kuiangalia kitaalamu na kupumzisha
ushabiki.
0 COMMENTS:
Post a Comment