January 17, 2015


Yanga itashuka dimbani leo Jumamosi kumenyana na Ruvu Shooting katika mchezo wa Ligi Kuu Bara lakini staa wa Yanga, Simon Msuva, ameandaliwa beki maalum wa kuhakikisha hafurukuti, huyo siyo mwingine bali ni George Michael.


George alikuwa tishio msimu uliopita ambapo alikuwa akiwadhibiti vizuri washambuliaji wengi wakiwemo Amissi Tambwe na Didier Kavumbagu huku akitumia nguvu nyingi kupambana.

Beki huyo aliwahi kunukuliwa akisema kuwa amekuwa akipiga ‘pushapu’ 100 kwa siku, hali ambayo alisema ilimsaidia kuwazima mafowadi.

Msemaji wa Ruvu, Masau Bwire, ameliambia gazeti hili kuwa, beki huyo amerejea na tayari ameshacheza baadhi ya mechi, huku akijinadi kuwa ndiyo atakuwa na kazi ya kuzima wasumbufu wa Yanga, akimtaja Simon Msuva kwa kuwa ndiye ambaye yupo kwenye kiwango kizuri.

“Msuva atawasumbua wengine ila siyo sisi, George amerudi na atakuwepo, huyu ndiye dawa ya wasumbufu siku zote na ndiyo kazi yake uwanjani,” alisema Bwire.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic