January 15, 2015


Unajisikiaje, kuona mpira wa Tanzania leo uko hivi tena katika karne hii?


Picha zinaonyesha mchezaji wa Polisi Dodoma akikimkimbiza mwamuzi wa mchezo wa Ligi Daraja la Kwanza dhidi ya Toto African.


Mwamuzi huo alilazimika kukimbia kwenye majukwaa ya Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza ambako aliokolewa na mashabiki waliompa kipigo mchezaji huyo.


Alimkibiza mwamuzi huyo baada ya kumpiga uwanjani lakini alipokimbia, aliona haitoshi akaendelea kumkimbiza.

Hii ndiyo soka ya Tanzania, bado wachezaji wanakimbiza waamuzi na kuwapiga.


Kweli kama wanakosea, sehemu sahihi za kuwapa adhabu zipo. Vipi wakimbizwe kama wizi? Hii ni aibu kubwa ka mpira wa Tanzania ambao ndiyo bado unavaa ‘nepi’ kutokana na udogo wake.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic