January 14, 2015


Baada ya kiungo mshambuliaji wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo, kuibuka Mchezaji Bora wa Dunia wa 2014, Kocha Mkuu wa timu ya taifa ya Tanzania (Taifa Stars), Mholanzi, Mart Nooij, ameibuka na kusema kuwa yeye kura zake alipiga kwa wachezaji watatu akiwemo nyota huyo.


Alitaja listi yake ya aliowapigia kura kuwa ni Arjen Robben (Bayern Munich), ya pili kwa Lionel Messi (Barcelona) na tatu kwa Cristiano Ronaldo, ambaye alikuwa akiitetea.

Kwa upande wa makocha, Nooij alichemka kwani katika listi yake alikuwepo Carlo Ancelotti (Real Madrid) ya pili ilikwenda kwa Louis van Gaal (Manchester United) na ya mwisho Pep Guardiola (Bayern Munich) wakati Fifa wamempa kocha wa Ujerumani, Joachim Low.

Nooij alisema aliwapigia wachezaji hao kutokana na kutambua umahiri na uwezo wao ambao ni wazi wanafanya vyema na siyo wababishaji wanapokuwa uwanjani, japo uwezo hauwezi kufanana moja kwa moja.

“Kura yangu ya kwanza nilimpigia Arjen Robben na wa pili alikuwa ni Lionel Messi na wa mwisho alikuwa Cristiano Ronaldo.

“Upande wa makocha nilimpa Carlo Ancelotti (Real Madrid), ya pili ilikwenda kwa Louis van Gaal (Manchester United) na nilimalizia kwa Pep Guardiola (Bayern Munich),” alisema Nooij.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic