January 9, 2015

MGOSI AKIMTOKA KIPA PETER MANYIKA WA SIMBA NA KUIFUNGIA MTIBWA SUGAR...
Hassan Mgosi, ambaye amekuwa na rekodi nzuri ya kuzifunga Simba na Yanga, amemtaja beki kisiki wa Yanga, Kelvin Yondani ‘Cotton’ kama mtu aliyempa mbinu za kuwatoka mabeki wanaokamia, enzi wakiwa pamoja Simba.


Mgosi amesema kuwa mbinu alizopewa na Yondani na Juma Nyosso ambaye sasa yupo Mbeya City, enzi walipokuwa Simba, zimemsaidia katika kuwapita mabeki wa timu kubwa, hasa za Simba na Yanga.

“Wakati tukiwa Simba, Yondani na Nyosso walikuwa wakifanya kila liwezekanalo kuhakikisha sifungi mazoezini, walikuwa wakicheza kwa kunikamia haswa na si utani, hali ile niliichukulia ‘serious’ nikawa nafanya juu chini ili nifunge, kumbe ilikuwa ikinijengea ujasili wa kutomuogopa beki yeyote hasa wanaokamia mastraika.

“Kwangu ulikuwa kama wosia maana nimekuwa nikifunga katika mechi za kukamia tofauti na nyingine,” alisema Mgosi ambaye yupo Unguja na timu yake kwa ajili ya Kombe la Mapinduzi.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic