January 14, 2015

Kocha wa Yanga, Hans van der Pluijm amesema anataka nafasi wanazotengeneza katika kikosi chake zitumite kutengeneza mabao.


Pluijm raia wa Uholanzi amesema itakuwa ni kazi bure kama watatengeneza nafasi nyingi na kushindwa kuzitumia.

“Soka ina kawaida ya kuendelea kukumbusha na wakati mwingine kufundisha jambo lilelile kwa mara nyingine tena.
“Lakini ninachotaka ni nafasi za kufunga mabao zitumike. Tunapotengeneza nafasi bila kuzitumia ni kazi bure,” alisema.

“Tayari nimezungumza na wachezaji wangu mara kadhaa na nitaendelea kuwakumbusha ili kuhakikisha kunakuwa na mabadiliko katika hilo,” alisema.

Yanga imekuwa na kikosi kinachopoteza nafasi nyingi za kufunga licha ya kushinda baadhi ya mechi kwa idadi nzuri ya mabao.


“Hata zile tulizoshinda kwa mabao manne, tulistahili kushinda zaidi,” alisisitiza Pluijm.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic