January 16, 2015

 Fernando Torres amefunga mabao mawili na kuiwezesha Atletico Madrid kutoka sare ya mabao 2-2 dhidi ya Real Madrid katika mechi ya Copa del Rey.


Kwa sare hiyo ndani ya Santiago Bernabeu, maana yake Madrid imeng’olewa kwa jumla ya mabao 4-2 baada ya kuwa imepoteza kwa mabao 2-0 katika mechi ya kwanza ikiwa ugenini.

Licha ya kuwa na wachezaji nyota zaidi duniani, Cristiano Ronaldo na Gareth Bale, Madrid ilishindwa kuonyesha cheche na kumzuia Torres kufanya mambo yake.

Torres amerejea Atletico akitokea AC Milan iliyomnunua kutoka Chelsea kabla ya kuamua kumpeleka Atletico kwa mkopo.









0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic