January 15, 2015


SANANI AKIZUNGUMZA...
Waandishi mbalimbali wa vyombo vya habari, wakiongozwa na wa gazeti la michezo la Championi na Azam TV,walionyesha mapenzi ya dhati walipoamua kumtembelea Masoud Sanani.


LUKONGE (KULIA) AKIWA NA MUWA NA MBULA WA AZAM TV
Sanani ni kati ya waandishi magwiji nchini hasa katika michezo na sasa ni mgonjwa baada ya kupooza upande mmoja wa mwili wake.

Waandishi hao walimtembelea nyumbani kwake eneo la Bububu mjini Zanzibar.


Waandishi hao walikuwa kwenye michuano ya Mapinduzi, kwa pamoja walifika kumuona gwiji huyo ambaye amewahi kufanya kazi katika makampuni ya Business Times akiwa na gazeti la Spoti Starehe  na Dar Leo kabla ya kuhamia Mwananchi ambako pia alifanya kazi katika Mwanaspoti.
LUKONGE WA CHAMPIONI AKISALIMIANA SANANI...

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic