February 21, 2015


Kiwango ambacho amekuwa akionyesha kipa wa Yanga, Ally Mustapha ‘Barthez’ kimewafanya wachezaji wenzake kukubali kuwa sasa amekuwa “mtamu” kuliko hata Mcharo wa Airtel.


Barthez alionyesha kiwango cha juu, juzi Alhamisi alipokuwa akiitumikia klabu yake ya Yanga katika Uwanja wa Sokoine mkoani hapa kwa kupangua michomo mikali iliyokuwa ikipigwa na washambuliaji wa Prisons.
Mpaka sasa, Barthez ameshacheza mechi sita bila kufungwa, ambapo ni sawa na kusema ametumia dakika 540 bila kuruhusu nyavu zake kutikiswa.
Hali hiyo iliwafanya baadhi ya wachezaji wenzake wammwagie sifa kwa kazi yake hiyo kwa kudai kuwa kwa sasa ndiye kipa bora hapa nchini kutokana na rekodi yake anayoishikilia.

Barthez anashikilia rekodi ya kufungwa bao moja tu katika mechi nane alizoitumikia klabu hiyo tangu alipoanza kupata nafasi katika kikosi cha kwanza cha timu hiyo mwanzoni mwa Januari katika michuano ya Kombe la Mapinduzi.

Nahodha wa Yanga, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, amesema kwa sasa Barthez ndiye kipa bora hapa nchini kutokana na kiwango chake cha juu anachoonyesha uwanjani tangu alipoanza kupata nafasi katika kikosi cha kwanza.

“Barthez kwa sasa yupo vizuri, anafanya kazi yake ipasavyo, hakika kwangu mimi hivi sasa ndiye kipa bora kwangu.”

Yeyey Barthez alisema: “Namshukuru Mungu kwani yeye ndiye anayeniongoza mimi kuwa katika kiwango hiki, lakini pia nawashukuru viongozi wangu wote wa benchi la ufundi kwa kuniamini na kuamua kunipatia nafasi hiyo, nitaendelea kujituma zaidi ili niweze kuwa bora zaidi siku zote.”


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic