February 20, 2015


Kipa wa Simba, Ivo Mapunda ambaye alisababisha hofu kwa wadau wa timu yake kutokana na kuchanika juu ya jicho katika mechi ya Ligi Kuu Bara dhidi ya Polisi Moro kwenye Uwanja wa Jamhuri wiki iliyopita, amepata nafuu na ameanza mazoezi pamoja na wenzake jana Alhamisi.


Mara baada ya kuumia, Ivo alitolewa uwanjani katika mchezo huo na kukimbizwa hospitali kwa matibabu zaidi kisha nafasi yake kuchukuliwa na Peter Manyika.

Daktari wa timu hiyo, Yassin Gembe, alisema hali ya kipa huyo kwa sasa ni nzuri na alianza mazoezi tangu jana Alhamisi baada ya maendeleo yake kuwa mazuri kwa kiasi kikubwa.

Gembe aliongeza kuwa, kwa upande wa beki wa timu huyo ambaye naye alipata majeraha ya mgongo katika mchezo huohuo wa Polisi, Hassan Kessy anaendelea vizuri.

“Kessy pia ameanza mazoezi kama kawaida baada ya kupata matatizo kidogo katika mchezo uliopita lakini sasa yupo fiti na wachezaji wengine kwa jumla wanaendelea vizuri,” alisema Gembe.


Simba inatarajiwa kukipiga dhidi ya Stand United kwenye Uwanja wa Kambarage ikiwa ni mwendelezo wa Ligi Kuu Bara.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic