February 20, 2015

MGOSI...
Baada ya kufanikiwa kupata ushindi wa mabao 2-0 mbele ya BDF XI, kupitia kwa straika mahiri wa kikosi cha Yanga, Amissi Tambwe, straika wa Mtibwa, Musa Hassan Mgosi ameibuka na kusema kuwa Tambwe ni hatari na ni mmoja wa wachezaji ambao kwake anaona wanastahili kuitwa bora nchini Tanzania.


Tambwe alifanikiwa kuzifumania nyavu mara mbili dhidi ya BDF XI, katika mchezo wa Kombe la Shirikisho uliopigwa wikiendi iliyopita kwenye Uwanja wa Taifa, Dar.
 
TAMBWE...
Mgosi amesema kuwa siku zote amekuwa akimkubali Tambwe kutokana na uwezo wake wa hali ya juu, hivyo alikuwa akimsubiri kwa hamu aifurahishe nafsi yake kama vile ambavyo alifanya wikiendi iliyopita.

“Ninapoitaja orodha yangu ya wachezaji bora Tanzania, Tambwe hawezi kukosa kwa sababu ni mchezaji ambaye ninamkubali sana, kikubwa amenifurahisha zaidi alipoifunga BDF XI.

“Ninawapongeza wachezaji wa Yanga kutokana na umoja wao waliouonyesha kwenye mchezo mbele ya wageni kutoka Botswana, nawaomba wasishibe sifa na wakafanye kweli kwenye mchezo wa marudiano wiki mbili zijazo,” alisema Mgosi.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic