February 20, 2015


Mkuu wa Wilaya ya Wanging’ombe Mkoa wa Njombe, Fredrick Wilfred Mwakalebela, ameahidi kuifanyia makubwa wilaya hiyo kwa kuanza na kuinua mchezo wa soka.


Kauli hiyo ameitoa ikiwa ni siku moja tangu Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, Dk Jakaya Kikwete kumtangaza kuwa mkuu mpya wa wilaya hiyo.

Mwakalebela ambaye ni katibu mkuu wa zamani wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), alisema wilaya hiyo ni mpya, hivyo anakabiliwa na changamoto kubwa ya kuhakikisha soka linapiga hatua wilayani humo.

Mwakalebela alisema wilaya hiyo ina mwamko mdogo katika soka, hivyo katika kuhakikisha anakuza mchezo huo, amepanga kuuinua kwa kuanza na shule za msingi na sekondari kwa kuwaanzishia mashindano ya wenyewe kwa wenyewe.

Aliongeza kuwa, pia amepanga kugawa vifaa mbalimbali vya michezo zikiwemo jezi, mipira, soksi na viatu kwa ajili ya kuchezea soka kwa wanafunzi.

“Kiukweli ninakabiliwa na changamoto kubwa ya kuhakikisha wilaya yangu inapiga hatua kwenye mchezo wa soka, hiyo ni kutokana na wilaya yenyewe kuwa mpya ambayo haina mwamko wa michezo.

“Kikubwa nitaandaa mashindano ya wenyewe kwa wenyewe mashuleni kwa kuanzia shule za msingi na sekondari, pia nitaandaa mashindano mengine mitaani kama yale ya Mufindi yaliyopewa jina la Muungano kwa kugawa vifaa vya michezo, ninaamini nitafanikiwa katika hilo kutokana na uzoefu wangu wa kuendesha soka nikiwa na TFF,” alisema Mwakalebela.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic