February 8, 2015



Kocha wa Chelsea, José Mourinho amesema anapaswa kupewa shukurani kubwa na taifa la Wafaransa kutokana na kuwapa nafasi wachezaji Frenchmen Raphaël Varane  na Kurt Zouma wakiwa na miaka kati ya 20na 21.


"Shirikisho la Soka la Ufaransa linapaswa kunipa shukurani kubwa kwa kuwa sasa wana mabeki wawili bora kabisa duniani. Mimi ndiyo nilitoa nafasi kwao ya kuwaamini,” alisema Mourinho.

Varane yuko Real Madrid ambako Mourinho alimuacha na alianza kumpa nafasi baada ya kufarakana na Pepe.
Licha ya umri wake mdogo wa miaka 20 lakini alimuamini zikiwemo kubwa na akafanya vema.


Zouma naye mwenye miaka 21, pia amekuwa akiendelea kupata nafasi katika kikosi cha Chelsea, hali ambayo imekuwa ikizidi kumuimarisha.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic