February 17, 2015


Kocha Mkuu wa Yanga, Hans van Pluijm amesema anaamini mchezo wa Ligi Kuu Bara kati yao dhidi ya Prisons mjini Mbeya utakuwa mgumu.


Pluijm ameungana na Kocha Mkuu wa Prisons, David Mwamwaja aliyesema kikosi chake ni kigumu na imara sana.

Lakini Pluijm raia wa Uholanzi amesema Yanga imeimarika katika kipindi hiki, hivyo Prisons wawe makini zaidi hata kama wako kwao.

“Wako ligi kuu, lazima tukiheshimu kikosi chao. Lakini kwa sasa kikosi chetu tayari kimekaa vizuri.

“Ninaamini wachezaji watakuwa katika ari ya juu, watacheza kwa umakini mkubwa. Sasa Prisons wasichukulie mambo kwa ulahisi,” alisema.


Yanga tayari imetua mjini Mbeya na Pluijm amesisitiza ana matumaini watafanya vizuri katika mechi hiyo ya Alhamisi kabla ya kuendelea kubaki na kuisubiri Mbeya City.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic