February 11, 2015


Yanga imesema kuwa haina mkanda wala haijaona mechi yoyote ya wapinzani wao BDF, lakini wanajua kuwa wana wachezaji kutoka Zambia.


Yanga itavaana na BDF XI ya Botswana keshokutwa Jumamosi lakini inasema itaingia kwa tahadhari zote kwa kuwa wageni hao ni bora sana.

Kocha msaidizi wa timu hiyo, Charles Mkwasa, ameliambia Championi Jumatano kuwa, wamejitahidi kadiri ya uwezo wao kuhakikisha wanapata video za timu hiyo ili waweze kuwaona lakini imeshindikana.

“Kuhusu wapinzani wetu hao hatuwajui ipasavyo, lakini tunasikia kuwa ni wazuri na wana wachezaji kama watatu hivi kutoka Zambia ambao wanadaiwa kuwa ni wazuri sana na wana akili sana uwanjani.


“Tumejitahidi kutafuta video zao ili tuweze kuwaona lakini imeshindikana, hivyo tumeamua suala hilo kuliachia uongozi na sisi tuendelee na kazi yetu ya kuhakikisha tunakuwa vizuri kwa ajili ya mechi hiyo,” alisema Mkwasa.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic