March 21, 2015


Kiungo mshambuliaji wa Yanga, Simon Msuva, amefungukia siri ya kung’aa katika kufumania nyavu kwa kusema kuwa, mazoezi binafsi anayoyafanya ndiyo sababu kubwa.


Msuva ambaye mpaka sasa amecheka na nyavu mara nane kwenye Ligi Kuu Bara, alisema mara nyingi amekuwa akifanya mazoezi ya kupiga krosi pamoja na vichwa, hali inayomfanya akiwa uwanjani apate urahisi zaidi wa kutupia.

“Licha ya kufundishwa na kocha Hans van Der Pluijm, lakini pia ninakuwa na mazoezi yangu. Naamini hayo yanachangia pia niweze kufunga nikisaidiana na wenzangu.


“Lakini kuhusu suala la mashabiki kunizomea, binafsi siliangalii suala hilo, bali ninachokiangalia ni kazi yangu niliyotumwa kufanya na uongozi, hivyo siwasikilizi hata kidogo kwani ukifanya vizuri ndiyo haohao wanaokushangilia.”

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic