March 23, 2015

Mashabiki wenye hasira wa Real Madrid wamelivamia gari aina ya Bentley lililokuwa linaendeshwa na kiungo Gareth Bale na kulipiga mateke na ngumi.

Mashabiki hao walikuwa na hamu ya kumvaa Bale wakidai hakuisaidia timu hiyo wakati ikicheza na Barcelona na kupoteza kwa mabao 2-1 kwenye Uwanja Camp Nou, jana.

Hasira zao zinatokana na kufungwa lakini ripoti ya magazeti ya leo ya AS na Marca zimeongeza chuki dhidi ya Bale.

Magazeti hayo yalionyesha Bale hakuwa na mchango hata punje huku yakikisitiza bei ya pauni milioni 86 aliyonunuliwa kutoke Tottenham, angalau ingetolewa robo yake tu wakati wa kumnunua.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic