March 25, 2015



Kiungo mshambuliaji wa Yanga, Simon Msuva amewaomba mashabiki wa Yanga kuendelea kuwaunga mkono.


Akihojiwa mara baada ya mchezo wa leo dhidi ya JKT Ruvu ambao alifunga mabao mawili, Msuva amesema anaamini wana kazi ngumu na wataendelea kufanya kama wataungwa mkono.

“Ushirikiano katika timu uko juu na tunataka kufanya vizuri. Lakini mashabiki watuunge mkono kwa kuwa inatupa nguvu ya kufanya vizuri zaidi,” alisema Msuva.

Kiungo huyo mwenye kasi wa Yanga amefikisha mabao 11 na kuongoza katika listi ya wafungaji bora.


Msuva amengoza kwa kumvuka Mrundi Didier Kavumbagu mwenye mabao 10 ambaye awali ndiye alikuwa kileleni.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic