March 29, 2015

SAID FELA (KUSHOTO) AKIWA NA TEMBA NA CHEGGE KATIKA MSIBA WA BONGE LEO.
Kifo cha mdau wa muziki na mwanzilishi wa kundi la Tip Top Connection, Abdul Bonge, kimeendelea kuzua utata baada ya jamaa aliyesababisha kifo chake aliyetajwa kwa jina la Nasoro kuingia mitini.

MAREHAMU ABDUL BONGE (KUSHOTO) WAKATI WA UHAI WAKE AKIWA NA FELA NA BABU TALE.

Akizungumza na mtandao huu mdogo wa marehemu aitwae Idd ambaye aliitwa kuichukua maiti ya kaka yake muda mfupi baada ya tukio alisema:

"Nikiwa na marehemu kuna kijana alimuita marehemu akagombelezee ugomvi wa Nasoro na mkewe na marehemu alipoenda kugombelezea ugomvi huo muda mfupi taarifa zilirudi kuwa Abdul alianguka na kupoteza fahamu.

“Nilikwenda kumuangalia nikamkuta ameanguka akiangalia juu huku ameng'ata ulimi, nilimkimbiza hospitali ya St Monica iliyopo Manzese Darajani ndipo nikaambiwa kaka yangu amepoteza maisha,” alisema. 

Mwili wa Abdul unatarajiwa kusafirishwea kupelekwa Kijiji cha Mkuyuni kilichopo Tarafa ya Matombo mkoani Morogoro baada ya taratibu za kipolisi kumalizika.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic