March 7, 2015


Yanga wameendelea kulikomalia suala la mshambuliaji wa Simba, Ibrahim Ajibu kucheza kwenye mchezo wa Prisons  akiwa na kadi tatu za njano na kusema lazima Simba wakatwe pointi tatu.


Sokomoko hilo limekuja baada ya TFF kuipa mamlaka Simba kumtumia Ajibu katika mechi na Prisons iliyopigwa wiki iliyopita huku pia ikimruhusu kucheza katika mchezo na Yanga hapo kesho wakati alitakiwa kutumikia adhabu kutokana na kuwa na kadi tatu za njano, lakini TFF kupitia kwa katibu na watendaji mbalimbali wamekuwa wakisisitiza kuwa kanuni zao zimefanyiwa marekebisho tangu Februari, mwaka huu.

Hata hivyo, Yanga pamoja na klabu za Azam, JKT Ruvu, Ruvu Shooting, Kagera Sugar na Coastal Union zimepinga kuwepo kwa mabadiliko hayo kwani hakuna taarifa rasmi iliyotumwa kwa klabu husika, zaidi ya Simba tu.

Katibu wa Yanga, Dk Jonas Tiboroha, amefunguka kuwa katiba barua hiyo kwenda TFF, wameambatanisha masharti matano na mojawapo likiitaka TFF, Simba kukatwa pointi sita na kupigwa adhabu kali kama fundisho.

“Hakuna taarifa zozote kuhusu kanuni kubadilishwa, iweje zianze kutumika ilhali hazijawafikia walengwa? Soka letu limekuwa likiendeshwa kienyeji zaidi lakini katika hili lazima tusimame kidete kutetea haki yetu.

“Bado tunajiuliza hayo mabadiliko yalifanywa lini na kwa sababu ipi ya msingi? Tumeamua kuwaandikia barua TFF na ninaipeleka leo (jana) na tunawapa maazimio yenye masharti matano kuhusu msimamo wetu. 

Mojawapo ni watendaji wa Bodi ya Ligi kujiengua kwa kushindwa utendaji, pili, Klabu ya Simba ipokwe pointi sita, maana kabla ya Ajibu walikuwa wamemtumia Banda (Abdi) kwenye mchezo na Coastal kimakosa, maana hakuna aliyejua kama kulikuwa kuna marekebisho ya kikanuni,” alisema Dk Tiboroha na kufunguka msimamo wao kwa Ajibu kucheza mchezo wa kesho.


“Sisi hatuna shida na mchezaji, wao wakitaka wamtumie maana watakuwa wanaturundikia pointi. Acheze tu, tutajua mbele kwa mbele.”

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic