April 28, 2015

Klabu ya AC Milan imetangaza nia ya kujenga uwanja wake mpya ambao unaaminika utakuwa wa kisasa zaidi.

Uwanja huo hautakuwa mrefu sana kwenda juu kwa kuwa sehemu yake ya uwanja itakuwa imechimbiwa chini tofauti na viwanja vingine.

Pia uwanja huo utakuwa na uwezo wa kuingiza watu 48,000 tu katikati ya hoteli kadhaa pamoja na majengo ambayo kutakuwa na maduka ya huduma mbalimbali yaliyouzunguka uwanja huo.

Imeelezwa kuwa uwanja huo hautakuwa ukiruhusu kelele za mashabiki kutoka nje na kuwasumbua wakazi wengine wa jiji la Milan. Utakuwa umejengwa katika uwezo wa kuzuia sauti hizo kutoka nje.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic