April 28, 2015


Mkuu wa kitengo cha habari cha Yanga ana mambo yake, sasa anawataka Simba wavae jezi za njano na kijani, ili wapate msaada.

Yanga imemaliza kazi kwa kutwaa ubingwa wa Tanzania Bara, hivyo Jerry Muro anaamini ni wakati mzuri wa kuisaidia Simba kama watakubali hayo masharti.

“Simba ni watani zetu, tunaweza kuwasaidia na hatuna matatizo hata kidogo. Kitu kikubwa wakubali kuvaa jezi za njano na kijani.

“Sisi tutawasaidia kumfunga Azam FC ili wao wapate nafasi ya pili.

“Haya ni masharti, wakikubali na sisi tutawasaidia. Nafikiri hilo liko wazi kabisa,” alisema Muro.
Muro amekuwa akiwaudhi Simba kutokana na neno lake la kusema ni “wa mchangani”.

Simba inapambana na Azam FC kuwania nafasi ya pili ili ishiriki michuano ya kimataifa msimu ujao.

1 COMMENTS:

  1. Mimi YANGA damu lakini nataka AZAM awe mshindi wa pili.
    AZAM kazeni buti.

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic