April 20, 2015


Kocha Msaidizi wa Simba, Selemani Matola, ametoboa kilichoifanya timu hiyo kupoteza mchezo wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Mbeya City uliopigwa juzi Jumamosi kwenye Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya ambapo Simba ilipigwa mabao 2-0.


Simba msimu huu imekuwa ‘mteja’ kwa Mbeya City. Katika mchezo wa mzunguko wa kwanza, ilikumbana na kipigo cha mabao 2-1 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar na juzi ikalambishwa dozi tena.

Matola alisema mchezo ulikuwa mzuri, lakini walikamatwa katika sehemu ya kiungo huku akiitaja pia ‘sub’ ya beki na nahodha wa timu hiyo, Hassani Isihaka aliyeumia, iliharibu mipango yao yote.

“Mchezo ulikuwa mzuri kiujumla kwa sababu ukiangalia Mbeya hawakutukamia sana, lakini tulikuwa na tatizo kidogo katika sehemu ya kiungo, wapinzani wetu ‘walituwini’ sana eneo hilo na kufanikiwa kushinda mchezo, tunawapongeza na tunajipanga upya kwa mchezo ujao.

“Sub ya Isihaka pia tulifanya bila kuipanga, kwa hiyo ikatuvurugia hesabu zetu, lakini ndivyo soka lilivyo, ‘sometimes’ tunatakiwa kukubali matokeo na kuangalia mipango ya mbele,” alisema kocha huyo aliyechukua jiko hivi karibuni.


Matokeo hayo yanaifanya Simba iifukuzie Azam kwa tofauti ya pointi saba katika nafasi ya pili, ikiwa imebakiza mechi nne kabla ya kumaliza ligi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic