April 20, 2015


Beki kisiki na nahodha wa kikosi cha Yanga, Nador Haroub ‘Cannavaro’, ametamka kuwa alipata wakati mgumu katika kumkabili straika wa Etoile du Sahel ya Tunisia, Bounedjah Baghdad kutokana na mshambuliaji huyo kuwa na uwezo mkubwa wa kupambana na mabeki.


Beki huyo ambaye alilazimika kutolewa uwanjani baada ya kuumia enka ya mguu wake wa kulia, ndiye alikuwa shujaa wa timu hiyo baada ya kufanikiwa kuifungia bao kwa mkwaju wa penalti katika mchezo huo ambao uliisha kwa sare ya 1-1.

Cannavaro alisema safu yao ya ulinzi ilipata wakati mgumu wa kukabiliana na mshambuliaji huyo kutokana na uwezo wake mkubwa aliokuwa nao wa kukabiliana na mabeki.

“Yule jamaa Baghdad achana naye kabisa kwani ni bonge la straika kutokana na kiwango chake kwa sababu anaweza kukaa na mipira, kupiga chenga na hata kukaa katika nafasi nzuri. Alitupa kazi kubwa katika kumkabili, jambo ambalo lilitufanya tutumie akili nyingi zaidi ya kumzuia.


“Lakini tunashukuru kwa kucheza naye ambapo hakuleta madhara makubwa kwa upande wetu ila alichangia kwa kiasi kikubwa katika majeraha yangu haya ya enka, ambayo nimeyapata,” alisema Cannavaro.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic