Licha ya kujituma na
kuhakikisha timu yao imebaki katika Ligi Kuu Bara, bado baadhi ya wachezaji wa
Ndanda FC wanadai fedha zao za malimbikizo ya mishahara na zile za usajili.
Wakizungumza kwa sharti
la kutotajwa, wachezaji hao ambao ni mashujaa kwa kuikoa timu hiyo kuteremka daraja walisema hawaelewi kwa nini hawalipwi
fedha zao wakati mara kadhaa Mbunge wa Mtwara Vijijini na Waziri wa Nchi, Ofisi
ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Hawa Ghasia,
amekuwa akitoa fedha.
Alipotafutwa Ofisa Habari
wa Ndanda, Idrissa Bandari, alisema: “Kweli tunadaiwa ila hatujui tutawalipa
lini hao wachezaji.”
0 COMMENTS:
Post a Comment