May 23, 2015


Licha ya kujituma na kuhakikisha timu yao imebaki katika Ligi Kuu Bara, bado baadhi ya wachezaji wa Ndanda FC wanadai fedha zao za malimbikizo ya mishahara na zile za usajili.


Wakizungumza kwa sharti la kutotajwa, wachezaji hao ambao ni mashujaa kwa kuikoa timu hiyo kuteremka daraja walisema hawaelewi kwa nini hawalipwi fedha zao wakati mara kadhaa Mbunge wa Mtwara Vijijini na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Hawa Ghasia, amekuwa akitoa fedha.


Alipotafutwa Ofisa Habari wa Ndanda, Idrissa Bandari, alisema: “Kweli tunadaiwa ila hatujui tutawalipa lini hao wachezaji.”

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic