June 17, 2015


Kocha Mkuu wa Kagera, Mbwana Makata, ameshindwa kuvumilia maneno ya watu wanaobeza Tuzo ya Kocha Bora wa Msimu aliyochukua wiki iliyopita kwa kusema kuwa kocha bora si lazima atwae ubingwa.

Mataka alijinyakulia tuzo hiyo mbele ya makocha, Hans van Der Pluijm wa Yanga na Goran Kopunovic wa Simba ambao walikuwa kwenye kinyang’anyiro hicho.

kocha huyo ambaye amejiunga na Kagera Sugar, alifunguka kuwa tuzo yake ilikuwa sahihi kwani bila yeye Prisons ingeshuka daraja.

“Nashukuru wote waliotambua kazi yangu ambayo binafsi nilikuwa shujaa. Niliikuta timu kwenye wakati mgumu sana, ilikuwa mkiani na pointi 13, kwa tofauti ya pointi 12, nyuma ya timu ya pili kutoka chini.

“Kila mmoja alikuwa akiniuliza kama ningeweza kuisaidia, lakini niliwajibu kuwa mimi ni daktari sina haja ya kuogopa hali ya mgonjwa. Nilipigana hadi ikabaki,” alisema Makata na kubeza kiaina ubingwa wa Yanga.


“Suala la kocha bora siyo lazima achukue ubingwa. Mbona England, Chelsea ilichukua ubingwa tena mapema sana, lakini kocha bora akachaguliwa wa Southampton (Ronald Koeman)? Kikubwa ni mchango wa mtu kwenye timu na si kigezo cha ubingwa.”

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic