Na Said Msumi
Safari
ya kuelekea mashindano ya mataifa huru ya Afrika (CAN) mwaka 2017 nchini Gabon
imeanza june 12 ambapo Tanzania ilitupa karata yake ya kwanza Juni 14 dhidi ya timu ya taifa ya Misri
’Mafarao’ ambapo katika mchezo huo Taifa
Stars ilikubali kichapo cha mabao 3-0, yaliyofungwa na Mohamed Salah, Basem Morsi na
Rami Rabia. Katika makala yangu mnamo Desemba 12, kichwa cha habari kilikuwa "Naanza kuchagua timu yangu ya Afcon sasa".
Niliezea kuhusu ushiriki wa timu ya taifa ya Tanzania taifa
stars kuhusu mashindano yanayokuja kwa mwaka 2017 hasa nikigusia upande wa
wachezaji,viongozi na mashabiki kwa ujumla.Lakini hebu tuangazie mambo kadhaa
tunaopaswa kuyaangalia katika mbio zetu kuelekea mashindano haya ya CAN.
Rekodi
Timu ya
taifa ya Misri inashika nafasi ya 55 katika viwango vya mpira duniani(FIFA)
kabla ya mchezo wa jumapili tumekutana mara nane huku tukipoteza michezo saba
na kutoka sare mchezo mmoja.Wadau wengi wamekuwa hawaamini kwenye upande wa
rekodi lakini bado timu hii ya misri ni kikwazo kwetu na tusipo angalia
tunaweza tukapoteza hata mchezo wa nyumbani.
|
05
Jun 1975
|
Tanzania
vs Egpty
|
1-1
|
|
01
Aug 1975
|
Egpty vs Tanzania
|
5-2
|
|
12
Mar 1980
|
Egpty vs Tanzania
|
2-1
|
|
04
Apr 1987
|
Tanzania
vs Egpty
|
2-4
|
|
17
Apr 1987
|
Egpty vs Tanzania
|
6-0
|
|
14
Oct 1994
|
Egpty vs Tanzania
|
5-1
|
|
22
Apr 1995
|
Tanzania vs Egpty
|
1-2
|
|
05
Nov 2009
|
Egpty vs Tanzania
|
5-1
|
|
05
Jan 2011
|
Egpty vs Tanzania
|
5-1
|
Nigeria
Timu
ya taifa ya Nigeria’super eagles’
yenyewe inashika nafasi ya 43 katika viwango vya FIFA ambapo yenyewe katika kundi G inashika nafasi ya pili baada ya
ushindi wa magoli 2-0 dhidi ya Chad. Bado rekodi yetu dhidi ya wababe hawa
Afrika sio nzuri hata kidogo hasa ikumbukwe mchezo unaofatia tunacheza nao
nyumbani mnamo September.
|
06
Jul 1972
|
Tanzania vs Nigeria
|
0-0
|
|
12
Jan 1973
|
Nigeria vs
Tanzania
|
2-1
|
|
08
march 1980
|
Nigeria
vs Tanzania
|
3-1
|
|
06
Dec 1980
|
Nigeria
vs Tanzania
|
1-1
|
|
20
Dec 1980
|
Tanzania vs Nigeria
|
0-2
|
|
11
sept 2002
|
Nigeria
vs Tanzania
|
2-0
|
Chad
Timu
hii taifa ya Chad ndio inaonekana kama kibonde katika kundi hili ambapo
katika viwango vya FIFA timu hii inashika nafasi ya 172 ambapo
ipo chini ya Tanzania lakini katika
michezo miwili tulikutana nao tumeweza kuwafunga kwao magoli 2-1 lakini na wao walitufunga 1-0
lakini si timu ya kubeza hata kidogo katika mashindano haya. Yenyewe inashika nafasi ya tatu katika kundi letu kutokana na kufungwa magoli
machache dhidi yetu.
TFF
Shirikisho
la mpira la Tanzania(TFF) nadhani wao kwa upande wao wamefanya kila kitu kwa
wachezaji na benchi la ufundi kwa sababu mosi wameiweka timu kambini zaidi ya
wiki mbili huko Ethiopia lakini pili timu hii iliweza kushiriki katika mashindano ya
Cosafa ili kuipa timu mechi nyingi za kirafiki lakini ingawaje tulikosa mechi
ya kirafiki katika kalenda ya Fifa lakini TFF kupitia kamati zake
za ufundi hasa mkurugenzi wa ufundi ambaye anahusika na uteuzi wa wachezaji wa
timu ya taifa kwa kushirikiana na kocha mkuu wanaweza wakapewa lawama kutokana
na uchaguzi wa wachezaji.
Swali la kujiuliza
mkurugenzi haoni wachezaji mbadala kwa baadhi ya wachezaji ambao hawafanyi
vizuri katika timu ya taifa?
Kocha
Kocha Mkuu,
Mart Nooij ameonekana kama hafai kuendelea kuifundisha timu yetu ya taifa lakini suala la kujiuliza wachezaji wetu wana
ubora wa kupambana na wachezaji kariba ya wamisri au Nigeria?
Kwa hapa
hatupaswi kumlaumu kocha lakini jambo ambalo kocha anapaswa kulaumiwa ni uteuzi
wa kikosi jambo ambalo alipingwa toka
awali tangia michuano ya Cosafa, si nia yangu kuwapigia chapuo baadhi ya
wachezaji lakini uwezo wao ulishahili
wawepo kikosini wachezaji kama Mohamed Husein ‘Tshabalala au Ally Mustapha
‘Barthez’ walitakiwa kuwa katika timu ya taifa nadhani hapa kocha anapaswa
kulaumiwa.
Lakini pia hata rekodi za mechi alizoziongoza sio nzuri hata kidogo
hapa anapaswa kupewa lawama pamoja na
benchi lake la ufundi kwa ujumla.
Wachezaji
Ukirejea
kwenye makala yangu nilitoa ushauri kwa wachezaji wetu kutambua thamani ya jezi
ya taifa pindi wanapovaa jezi hiyo nadhani wachezaji wanapaswa kucheza zaidi ya
uwezo wao mathalani mchezo dhidi ya Cameroun kwao mjini Younde tuliopeteza kwa mabao 2-1 au dhidi ya Burkina Faso katika mji wa Ouagaduoguo tulioshinda bao1-0 au
tuliopoteza dhidi ya Ivory Coast kwao mabao 2-0.
Hata kama tulipoteza kila mtu
alihamasika na kiwango cha wachezaji nadhani wachezaji wanapaswa kubadilika kwa
sababu wao ndio wenye jukumu la kuleta mafanikio na sio kocha.
Nadhani
sasa ni wakati mzuri kwa TFF kuwashirikisha wachezaji wa zamani katika timu ya
taifa ilikuwasaidia kuwapa ujuzi zaidi mana sasa mchezaji wa zamani ni mmoja tu
ambaye naye ni meneja Tasso Mukebezi lakini pia serikali,wadau muda ni sasa
kujipanga mapema mana mechi dhidi yetu
na Nigeria sio mbali maandalizi ya uhakika yanahitajika mapema na sio kuwatupia
lawama baadhi ya wachezaji kama Oscar Joshua na wengineo.
Mwandishi
wa makala hii ni mwanafunzi wa mwaka wa kwanza katika Shahada ya Mahusiano kwa
umma- UDSM
0654-234573








0 COMMENTS:
Post a Comment