MURO |
Mkurugenzi wa Kitengo
cha habari cha Yanga, Jerry Muro amevunja ukimya na kujibu dongo la Haji Manara
wa Simba kwa kusema Yanga wanajiamini.
Muro amemjibu Manara
ambaye ni Mkuu wa Kitengo cha Habari cha Simba kwa kumuambia Yanga si wachawi,
hivyo hawana sababu ya kufanya mambo yao kwa kificho.
MANARAManara alikaririwa akijitapa jana kwamba Simba inafanya mambo yake kwa uficho mkubwa, si kama wenzao (Yanga) ambao kila kitu chao kipo kwenye vyombo vya habari. |
“Tuna haja gani ya
kuficha, wachezaji wawili kutoka Ghana na Zimbabwe wamekuja, tumewafanyia
vipimo na mwisho wameingia mkataba.
“Hatuna sababu ya
kuficha jambo, tunajiamini. Sisi si wachawi kufanya mambo kificho. Wenzetu
huenda hawana fedha.
“Au inawezekana usajili
wao una mambo ya figisufiisu, hivyo wanataka kuficha,” alisema Muro.
Yanga imefanikiwa
kuwasajili Donald Ngoma na Joseph Zuttah ‘Tetteh” kutoka Ghana na kukamilisha
idadi ya wachezaji saba wa kulipwa.
0 COMMENTS:
Post a Comment