July 28, 2015

PICHA ALIYOITUPIA MACHUPPA MTANDAO IKIMUONYESHA LOWASSA NA VIONGOZI WENGI WA JUU WA CHADEMA.

Mshambuliaji wa zamani wa Simba, Athumani Machuppa ‘Mani’ ameonyesha wazi hisia zake kutokana na taarifa za kuwa mwanasiasa mkongwe wa CCM, Edward Lowassa anahamia upinzani.

Machuppa anayeishi nchini Sweden ametupia picha aliyoiunganisha kutoka mtadao wa kijamii wa Twitter na kuiweka Facebook huku akisema: “madaraka haya”.

Katika maelezo yake, Machuppa anaonyesha kushangazwa na Lowassa kuhamia Ukawa ambao wapinzani ndiyo waliomuita fisadi.
 MACHUPPA.

Asilimia 90 wanaonekana kumuunga mkono Machuppa huku wakishangazwa na Lowassa anayeungana na waliomuita fisadi na mwizi.

Lakini wengine wanamuunga mkono Lowassa kwamba CCM zaidi ya miaka 50 sasa hawajaleta maendeleo.
Mwisho Machuppa anonyesha kuhoji, kwamba kama hakuna maendeleo, Lowassa atayaleta? Swali lake linaonekana kuwa gumu.

Taarifa hiyo huku picha inaonekana Lowassa akiwa na viongozi wa Chadema imezua stori nyingi mtandaoni na watu wanajadili hasa suala la wapinzani kumtangaza Lowassa ni fisadi na sasa wanakubali awe mgombea wao wa urais?

4 COMMENTS:

  1. Machupa aachane na siasa acheze mpira kila mtu na fani yake... au amesahau kuwa siasa na mpira ni vitu tofauti? Kila mtu anayo hiyari ya kuhama chama kwani chama si kabila au mmesahau hata Nyerere aliwahi kusema CCM si BABA wala MAMA YAKE?

    ReplyDelete
  2. Nchi hii kila mtu ana uhuru wa kutoa maoni yake,nionavyo mimi Machupa ametoa yaliyo moyoni mwake kuhusiana na sakata la Lowassa kuhamia upinzani tena CHADEMA,Kwangu Mimi angehamia chama chochote cha kisiasa cha upinzani tofauti na vyama ambavyo vilimuita majina kede wa kede machafu wala nisingeshtuka,,Sasa kuhamia kule kule kwa balozi na kuanza kusafishwa hapo kwangu ndio tatizo,kwani inaonesha Chadema hawana candidate anaefaa kuwania Uraisi na kuitoa CCM madarakani?

    ReplyDelete
  3. Ah ,kila mtu anaona,nionavyo hawa viongozi wetu njaa zita waua

    ReplyDelete
  4. Kastaafu mpira sasa hv jamani ana haki ya kuchangia kama mtanzania lowassa nani bwana sisi tulitegemea sura mpya kumbe kuna kitu anataka mamvi pale magogoni watch out..

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic