July 18, 2015


Straika mpya wa Simba, Hamis Kiiza, amesema atahakikisha anaitumikia ipasavyo timu yake mpya na kuipa mafanikio kama alivyofanya wakati anaichezea Yanga.

Kiiza amejiunga na Simba hivi karibuni na kupewa mkataba wa miaka miwili baada ya kuachwa na Yanga katika dirisha dogo la usajili Desemba, mwaka jana.

 Kiiza amesisitiza atajitahidi kwa kadiri ya uwezo wake kuisaidia Simba ifikie malengo yake na atacheza kwa kiwango kikubwa kama alivyofanya awali.

“Nipo Simba na nawaahidi mashabiki wasiwe na wasiwasi juu ya kuisaidia timu hii kwenye suala zima la kupata mafanikio,” alisema Kiiza na kuongeza:


“Nitajitahidi kuhakikisha vile nilivyofanya nikiwa na Yanga navihamishia huku kwa sababu nimeondoka kule sikuwa na deni hata moja kwani mataji niliwapa.”

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic