July 20, 2015


Kocha wa zamani wa Simba, Patrick Liewig raia wa Ufaransa ametua nchini na rasmi kutambulishwa kuwa kocha mpya wa Stand United.

Liewig ambaye aliifundisha Simba kwa nusu msimu, anatarajia kusaini mkataba wa miaka mitatu kuinoa Stand United ya Shinyanga.

Mkurugenzi wa ufundi wa Stand United, Muhimu Kanu amesema kila kitu kimekwenda vizuri.

“Limebaki suala la kusaini mkataba tu, litafanyika leo jioni na matarajio yetu kila kitu kitakwenda vizuri,” alisema Kanu.

Stand ambayo imeingia mkataba wa mamilioni ya fedha na kampuni ya uchimbaji madini ya Acasia, imepania kujiimarisha zaidi kwa ajili ya msimu ujao wa Ligi Kuu Bara.


Msimu huo utakuwa wa pili kwa Stand United iliyocheza msimu uliopita ingawa mwishoni ililazimika kufanya kazi ya ziada kupigania ‘roho’ yake ili ibaki.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic