July 18, 2015


Timu ya soka ya Jeshi la Rwanda, APR leo Jumamosi saa 8:00 mchana inacheza mechi ya kwanza ya Kombe la Kagame dhidi ya Al Shandy kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, kikosi hicho kimedai kiungo wake Jean Baptiste Mugiraneza ‘Migi’ amewaharibia.

Hiyo ni kauli ya Kocha Msaidizi wa APR, Vincent Mashami wakati alipokuwa akielezea mchezo wao wa leo wa Kundi B dhidi ya Al Shandy ya Sudan.

“Unajua Migi alikuwa mchezaji wetu tegemeo na nahodha, sasa kuondoka kwake kumetufanya tuwe na pengo kikosini, amevuruga mipango yetu ya kutwaa ubingwa.

“Hata hivyo, tutapambana na wachezaji tulionao ili tuweze kufanya vizuri, kwani kumkosa Migi ni mambo ya kiuongozi zaidi ndiyo yaliyotokea” alisema Mashami.


Migi amejiunga na Azam FC siku chache zilizopita lakini kutokana na majeraha ya jino aliyopata katika mazoezi ya timu hiyo, hatacheza mechi ya kesho ya Kombe la Kagame itakayoikutanisha Azam na KCCA.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic